• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
BARIADI TOWN COUNCIL
BARIADI TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri Ya Mji Bariadi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhima na Dira
    • Historia
  • Huduma
    • Leseni za Biashara
    • Hati za Viwanja
    • Tozo za Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
    • Kitengo
  • Machapisho
    • Fomu
    • Ripoti
    • Habari
    • Waraka
    • Sheria
    • Sera
    • Gazeti la Serikali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
  • Miradi
  • Tangazo
  • Michezo na Burudani
  • Zabuni

Masharti ya Kupata Leseni za biashara


LESENI ZA BIASHARA (Business Licensing Act No 25 of 1972, Amendment 1980 and 2014)

MASHARTI YA KUPATA LESENI YA BIASHARA

Mtu yeyote raia wa Tanzania anayo haki ya kupatiwa leseni ya biashara ili mradi awe  ametimiza  umri wa  miaka  kumi  na  nane  (18) mwenye  akili  timamu  na ambaye hajawahi kupatikana na kosa la jinai (katika kipindi cha miezi 12 iliyopita) na awe na eneo la kufanyia biashara linalokubalika kisheria.

Kwa mtu ambaye sio raia wa Tanzania anapaswa kuwa na Hati ya kuishi nchini daraja `A`(Residence permit class A) na nyaraka nyingine za usajili wa kampuni yake ndio aweze kufanya biashara nchini.

UTARATIBU WA KUPATA LESENI YA BIASHARA

Mwombaji anapaswa kujaza fomu ya maombi TFN 211 kikamilifu na kuambatanisha kivuli cha:-

(i)        Certificate of Incorporation iwapo ni kampuni na Certificate of

Registration and Extract kama ni jina la biashara.

(ii)      “Memorandum and Article of Association”ambayo inaonesha kipengele ambacho kampuni hiyo inakiombea leseni ya biashara..

(iii)      Passport ya Tanzania au Kitambulisho cha uraia au Kitambulisho cha mpiga  kura  au   Cheti   cha   kuzaliwa   au   Hati  ya   kiapo(affidavit) kuonyesha kuwa ni Mtanzania na Mgeni Hati ya kuishi nchini daraja la “A” (Residnece Permit Class “A”).

(iv)     Hati  ya  kiuwakili  (Powers  of  attorney)  Iwapo  wenye  hisa  wote  wa Kampuni  wapo nje ya  nchi,itolewe  kwa  mtanzania ambaye  anaishi hapa.

(v)        Ushahidi wa maandishi kuwa ana mahali pa, kufanyia biashara (Kwa mfano hati za nyumba, mkataba wa upangishaji, risiti za malipo ya kodi za majengo au ardhi.

(vi) Hati ya kujiandikisha kama mlipa kodi TRA (TIN).

(vii) Kwa leseni zinazodhibitiwa na Mamlaka mbalimbali, Kwa mfano (TFDA, EWURA, ERB, TPRI, TCRA, CRB, TALA, CAL) n.k lazima mwombaji kuwa na leseni husika kabla ya kuomba leseni ya biashara.

(viii) Hati za utaalam (Professional certificates) kwa biashara zote za kitaalam mfano Ushauri wa kitaalam (Consultancy), udaktari, urubani wa ndege, uhandisi nk.

Maombi mapya yanapitia ngazi zote za mwanzo kwa ajili ya ukaguzi kabla ya kupitishwa au kupatiwa leseni, ambazo ni Afya, Mipango miji na Afisa biashara wa kata au eneo ambapo biashara husika inayoombewa leseni itafanyika.




MAKOSA YA LESENI ZA BIASHARA.

i.         Kuendesha biashara bila leseni.

ii.         Kuendesha biashara  eneo  tofauti  na  linaloonyeshwa  kwenye leseni.

iii.        Kutumia leseni moja kufanyia biashara zaidi ya moja au maeneo mawili au zaidi.

iv.       Kushindwa  kuonyesha  leseni  ya  biashara  inapotakiwa  kufanya hivyo na Afisa  aliyeidhinishwa na Serikali.

v.         Kutokuweka leseni ya biashara mahali ambapo inaonekana kwa urahisi.

vi.       Kutoa  maelezo  ya  uongo  ili  kupata  leseni  au  kukwepa  kulipa ada/kodi inayostahili.

vii.      Kumzuia Afisa wa Serikali aliyepewa mamlaka ya kukagua kufanya kazi yake.

ADHABU

Mtu yeyote anayetenda majawapo ya makosa hapo juu adhabu yake ni faini isiyopungua Tshs. 50,000/= na isiyozidi Tshs. 100,000 au kifungo kisichozidi

miaka miwili (2) au faini na kifungo kwa pamoja.

MASHARTI YA UTUMIAJI WA LESENI

1.  Mwenye leseni hataweka masharti yeyote kwa mnunuzi.

2.  Mwenye leseni atatoa risiti kwa mauzo yote.

3.  Mwenye leseni atafuata sheria ya leseni ya Biashara No. 25 ya 1972 na marekebisho yake.

4.  Mwenye leseni hatatowa huduma/bidhaa ambazo hazizingatii viwango vya ubora,uliowekwa na vyombo vinavyotumika kisheria.

5.  Mwenye leseni anaweza kunyaganywa leseni na mamlaka iliyotoa wakati wowote ikiwa itaonekana aliipata kwa njia ya danganyifu au amekiuka msharti ya leseni.

ANGALIZO:

LESENI ZA BIASHARA HULIPIWA ADA NA KUHUISHWA (RENEW) KILA MWAKA KWA MJIBU WA SHERIA YA LESENI No. 25 YA 1972 NA MAREKEBISHO YAKE YA 2014). MFANYABIASHARA   ANATAKIWA KUHUISHA LESENI YAKE YA BIASHARA NDANI YA SIKU 21 TANGU ILIPOMALIZIKA NA PENALTY YA 25% ITATOZWA KWA WANAOCHELEWA NA ITAKUWA IKIONGEZEKA KWA 2% KILA MWEZI.

VIWANGO VYA LESENI ZA BIASHARA






SIN              COLUMN)                          COLUMN    11                 COLUMNlTI              COLUMN   IV

BUSINESS                           BUSINESS CATEGORY                     DESCRIPTION
FEE FOR
PRINCIPAL LICENCE

FEE FOR

SUBSIDIARY LICENCE

Local

300,000=
200,0001=
Foreian Owned
3,000  USD
1,500 USD
7. Medical  Practitioner


Local

Foreign

150,000/=
1,000  USD
15o,bOOI=
1,000  usn
8.J\ny  other  consultancv


Local

200,000/=
100,0001=



Foreign   Owned
3,000  US!)
2,000  US])



9. If employees   of

NIL

NTL



government,   Parastatal





Organization





Religious   owned,





institution   or Private





companies


10
General
Trading
I. Dispensary,   health
RO,OOO/-
50,000/=



centre  and  Laboratory





Clinic





2. Hospital-         Local


150,000/=


100,000/=


._             -




Foreign                                            1,000  US))                  1,000  US))

3. Selling  Medicines retail

(a)parl   i poison  shop                    200,0001-                  100,0001=

-;

(blPart  ii poison  shop                  100,000/-                       80,000/=

4. Hardware   and

Building   materials   retail

(a) City  I Municipal                       200,0001=                 150,000/= (h) District                                       150,000/=                     100,0001=- (c) Minor  settlement   and              60,000/-                        50,000/=

Village                                                                                                     -_.    -

5. Workshop   & Garages

(a)  City / Municipal                        150,0001-                 100,000/= (b) District                                       120,0001=                 100,0001= (c) Minor  settlement   and             100,0001-                      50,000/=

Village




6. Bakeries


3U,UOO/-                  30,000/=




(a)  City / Municipal                        100,000/=                      50,000/=








SIN            COLUMN  I


COLUMN    11


COLUMN  III


COLUMN-IY._]




BUSINESS

C.I\TEGORY


BUSINESS                     FEE FOR

DESCRIPTION               PRINCIPAL

_         r "CENCE


FEE  FOR

SU8SlI>IARY

LICENCE




---       --   - --  -1-------

.       1_1_ Auctioneers

'----


!2Q,OOOI=_


I 50,(lOO/'--




12    Seilingspar-c-pa-n-s.·-'-I-'-I--------          -  --------

•  JV   otor Vehicle -----




(a)  Cit~MLlnidpal              _

_(b)  I )istrict

(c) Minor settlement and

Villatic  .   _


300,O(Xl/-=

2S0]lOO!=

30,(KJO/=


200,COO/-'

ISO,(lO()f--

30,000/





2. M01~~)'cks

i.~_Cily !Ml~!~iIXII _                120,()()O/ (b)  DIstrict                                  llO,O()()/-- ( c)   Minor  settlement           -   -;J-6,6oo/=

and Villa~                                                 _


IOO,OO()/ SO,DUO!

30,(X)()/





3.Bic~                       _ (a) City I MUnlcipal JQll)istrict     _

( c)   MinOT sct~el1len~ (d)Villagc

--        -------

·1. Industrial SparesmId

Tools

(~2Cit)' I_~~!}_i~il)ul

(b)  District

(c ) Minor scttle;;';-;m

and Yillu8£


-50,0001=-           --     -

---    -

.      -30-,0_001=.-

lO,ODO/=

---S:<)()O/=

JOO,OOO!:

2S0,O()O/o:: IOO,nOD/::


30,0001=

20,(){)O/=

IO,OOO'=---

5,O(X)/=

21l0,(X)O!'-

150,000/-

---so ,oooi;;-





5_  Agr-icUltural   - implements, Flour Mills,

Machme$ spares                               _

(a) City / MlIni<:p~        _ ~,O()O/=

(b)   District                                  GO,000/= (c)   Minor settlement                 20,O()O!= and ~l~                          .                   _


uiO,O(lOr;-  --

30,000/=

10,000/-'





6 . Marine spares and tools

_(~ CitY.J_~unicipa)_


------ -

2S0,(X)0/=


150,000/=--    --




l~)J2!:!..'!:J~\


_         . _   ~_   200,(XlO/=


100,000/.:





=

No.2                                                   Finance                                                          2014

I



SIN
COLUMN
I
COLUMN    Jl
COLUMN  III
COI.llMN     IV

BUSINESS

BUSINESS
FEE  FOR
FEE  FOR


PRINCIPAL               SUBSID1ARY CATEGORY                      DESCRIPTION                       LICENCE                    LICENCE


(e )DcEartmcntal   stores
1 Cuv / Municipal
400,OOOi=
300,000/=
2 District
200,000/=
200,000/=
15
Endorsement
on
City,  Municipal,   District,
10,000/=
10,000/=

Transfer licenses

Minor  settlement  and villages


16    Duplicate   license           City,  Municipal,   District, for lost one                     Minor  settlement   and

villages                                              20,000/=                       10,000/=

·17     lilly  other  business        City  I Mnnicieality                          80,000/=                       60,000/= not of national   or          At District  headquarter                   50,000/=                       40,000/= international    nature       In Minor  Settlement                        IS,()OO/=                     15,000/=

-          At village                                           5,000/=                         5,000/=

20

--    --  --  ---------------------------




LESENI ZA VILEO ( The Intoxicating Liquors Act No.28 of 1968,Amendment No. 27-

1968,CAP 77 R.E.2002 ,Intoxicating liquors Licence fees order 1996 section(101).

Sheria ya leseni za vileo imenyambulisha aina tisa za leseni za vileo zinazoweza kutolewa chini ya sheria hii:

RETAILERS ON

Leseni  hii  humruhusu  mwenye  biashara  kuuza  pombe  na  kunywa  eneo  la biashara

RETAILERS OFF

Leseni  hii haimruhusu  mtu  kinywea  pombe  eneo  la  biashara  bali  kwa  watu wanaochukua kunyewea majumbani (Take away) kama Groceries.

WHOLESALE

Leseni hii ni kuuza pombe kwa jumla

HOTEL

Leseni hii humruhusu mwenye leseni kuuza pombe kwa ajili ya kunywea katika eneo la biashara kwa watu waliopanga hotelini kwa wakati wowote wa mchana na usiku

RESTAURANT

Leseni hii inamruhusu mwenye leseni kuuza pombe kwa mtu yeyote anayekula chakula  katika  mgahawa  katika  muda  wa  saa  6.00  mchana  hadi  saa  8.00 mchana na saa 12.00 jioni hadi saa 6.00 usiku.

MEMBERS CLUB

Leseni hii huruhusu uuzaji wa pombe kwa kiasi chochote kwa mwanachama wa

Klabu na wageni wao tu.

COMBINED

Leseni ambazo zimeambatanishwa mhili kwa pamoja:

(a)  Combined Hotel and retailers on

(b)  Combined Hotel and Restaurant

(c)  Combined restaurant and retailers on

TEMPORARY

Leseni hii humruhusu mwenye leseni kuuza pombe katika sehemu iliyotajwa kwenye leseni mahali penye burudani, starehe au mkusanyiko mwingine kwa kipindi kisichozidi siku tatu




LOCAL LIQUOR

Class A Local Liquor

Leseni hii humruhusu mwenye  leseni kutengeneza  pombe  za  kienyeji katika sehemu iliyotajwa na kuuza kwa ajili ya kunywea sehemu ya biashara au nje ya sehemu ya biashara

Class B Local Liquor

Leseni  hii  humruhusu  kutengeneza  pombe  ya  kienyeji  sehemu  iliyotajwa  na kwenda kuuzia sehemu nyingine iliyo na leseni ya kuuza pombe za kienyeji

Class C Local Liquor

Leseni hii humruhusu kutengeneza pombe ya kienyeji katika sehemu iliyotajwa kwenye leseni na kuuza kwa mwenye class D au Class E

Class D Local Liquor

Leseni hii humruhusu kuuza pombe za kienyeji katika sehemu iliyotajwa kwenye leseni kwa kunywea eneo la biashara

Class E Local Liquor

Leseni hii humruhusu kuuza pombe za kienyeji kwa ajili ya kunyewea sehemu nyingine mbali ya eneo la biashara

1.  MASHARTI YA KUPATA LESENI YA VILEO

Mtu yeyote raia wa Tanzania anayo haki ya kupatiwa leseni ya

Vileo ili mradi awe ametimiza umri wa miaka kumi na nane (18) mwenye akili timamu ambaye hajawahi kupatikana na kosa la jinai na awe na eneo la kufanyia biashara linalokubalika kisheria.

Kwa mtu ambaye sio raia wa Tanzania anapaswa kuwa na kibali kinachomruhusu kufanya biashara nchini kutoka Idara ya Uhamiaji.

2.  UTARATIBU WA KUPATA LESENI

•   Mwombaji hujaza fomu za maombi zinazotolewa na Manispaa  au kwenye

            mtandao wa Manispaa. 

•   Eneo/jengo linalokusudiwa kufanyia biashara hiyo kukaguliwa na Afisa

Afya, Afisa Mipangomiji, Polisi, Afisa Mtendaji wa Kata (WDC) na Afisa

Biashara wa Manispaa na hutoa maoni yao kwenye fomu husika  

 

•   Maombi hayo hupelekwa katika Malaka ya Utoaji wa Leseni za Vileo ya

            Manispaa kwa uamuzi 

•    Mwombaji ambaye maombi yake yamepitishwa hupewa Leseni baada ya

kulipa ada inayotakiwa na ni lazima amekamilisha masharti.




VIWANGO VYA ADA ZA VILEO

Viwango vya ada vinavyotumika kwa sasa kwa aina mbalimbali za leseni ni kama zifuatavyo:-

1. Retailers On  (Baa)
- 30,000.00  hadi
40,000.00
2. Retailers Off  (Grosari)
- 20,000.00  hadi
30,000.00
3. Wholesale (Jumla)
- 10,000.00  hadi
20,000.00
4. Members Club (Klabu Wanachama) -
10,000.00  hadi
20,000.00
5. Restaurant & Retailers On
-   30,000.00 hadi
40,000.00
6. Temporary licence (Leseni ya muda) -
7,000.00 hadi
15,000.00
7. Hotel Licence (Leseni ya Hoteli)
- 30,000.00 hadi
40,000.00
8. Retailers Off non-spirituous
-    7,000.00 hadi
15,000.00
9. Retailers On – non-spirituous
-   10,000.00 hadi
15,000.00

Mamlaka ya Vileo itaamua kiwango cha ada kitakachotozwa kati ya kiwango cha chini na kile cha kima cha juu. Viwango vinavyotumika kwa sasa na Manispaa ni vile vya kima cha juu kwa kila aina ya leseni.

3. MASHARTI YA UTUMIAJI

Leseni za vileo zina masharti mengi ikiwa ni pamoja na kutouza kilevi

kwa watoto. Masharti mengine ni muda wa kuuza pombe,kelele za muziki na kuwa na eneo la maegesho.

MUDA WA KUUZA POMBE( Act No 27 (1) a

BAA (RETAILERS ON)

      •   Jumatatu hadi Ijumaa - Saa 12.00 jioni hadi saa 5.00 Usiku  

•   Jumamosi, Jumapili na Sikukuu - Saa 5.00 asubuhi hadi saa 8.00 mchana

na saa 12.00 jioni hadi saa 6.00 usiku  

GROSARI (RETAILERS OFF)

•   Jumatatu hadi Ijumaa - Saa 2.00 asubuhi hadi saa 1.00 jioni  

•   Jumamosi, Jumapili na Sikukuu - Saa 3.00 asubuhi hadi saa 6.00mchana.  

RESTAURANT LICENCE (MGAHAWA)

•   Jumatatu hadi Ijumaa - Saa 6.00 mchana hadi saa 8.00 mchana  

na saa 12.00 jioni hasi saa 6.00 usiku

•   Jumamosi, Jumapili na Sikukuu - Saa 5.00 asubuhi hadi saa 8.00  

mchana na saa 12.00 jioni hadi saa 6.00




usiku

MAKOSA

Baadhi ya makosa chini ya sheria hii:

•   Kuruhusu  biashara  nyingine  isiyokubalika  kisheria  kufanyika  eneo  la

            biashara  

•   Kuuza pombe kwa mtu mwenye umri chini ya miaka kumi na sita (16)  

 

      •   Kuajiri mtu chini ya miaka kumi na sita (16) kuuza pombe  

•   Kuruhusu mtu mwenye umri chini ya miaka kumi na sita kukaa eneo la

            kuuzia pombe  

•   Kutoweka leseni sehemu ya wazi, ambapo itaonekana kwa urahisi na

            wakaguzi  

•   Kumruhusu/kuleta fujo katika eneo la biashara  

      •   Kuruhusu eneo la biashara kutumika kama danguro  

      •   Kuuza pombe muda ambao ni kinyume cha sheria  

•   Kufanya biashara ya pombe kwa kutumia leseni ya vileo ambao haistahili  

 

ADHABU

Mfanyabiashara  anayetenda  mojawapo  ya  makosa  haya  akikamatwa, atafikishwa mahakamani na akitiwa hatiani atalipa faini au kifungo au adhabu zote kwa pamoja.

UTARATIBU WA USHURU WA MALAZI (HOTEL LEVY) CHINI YA SHERIA NA. 23 YA 1972

MASHARTI YA KULIPIA HOTEL LEVY

1.  Kila mmiliki wa nyumba ya wageni (Guest House) anapaswa kulipa kodi ya asilimia ishirini (20) ya malipo ya nyumba (Guest House charges) kwa mwezi husika. Wamiliki wenye mauzo yanayotozwa kodi ya zaidi ya Tshs.

40 milioni kwa mwaka hawatalipa kodi ya malazi bali watalipa Kodi ya

ongezeko la thamani (VAT) .

2.  Kodi iliyowekwa, italipwa kuanzia tarehe moja hadi tarehe saba ya mwezi unaofuata mauzo

UTARATIBU WA KULIPIA HOTEL LEVY

•    Malipo  ya  Ushuru  wa  Malazi  ni  lazima  yaambatanishwe  na  fomu  ya mapato ya kila siku (fomu H.L. 1) au kitabu cha wageni, na fomu ya mapato ya kila mwezi (fomu H.L.2)  

•    Mmiliki wa nyumba analeta fomu H.L.1 au kitabu cha wageni pamoja na fomu H.L. 2 ambaye amekwisha jaza. Afisa anayekadiria atapitia H.L.1 au kitabu cha wageni na fomu H.L. 2 ili kuhakikisha ni sawa na kuhakikisha mmiliki amefikia vizuri asilimia 20 ya mapato ya malazi ya mwezi.  

 

 

     •   Mmiliki akishindwa kulipa ushuru kwa muda uliopangwa, siku saba  

(7) baada ya mwezi husika kumalizika, atalipa nyongeza ya asilimia  

25 ya ushuru unaotakiwa kulipwa, na endapo ataendelea kutokulipa adhabu (penalty) itakuwa inaongezeka kwa asilimia kumi (10) ya ushuru uliotakiwa kulipwa kila baada ya siku thelathini (30) kumalizika

MAKOSA

•    Mmiliki wa nyumba ya kulala wageni kushindwa kulipa ushuru wa malazi kwa muda unaotakiwa  

•   Kushindwa au kukataa kuwasilisha fomu ya mapato ya kila mwezi  

•  Kushindwa  kuweka  na  kutunza  kitabu  chenye  kumbukumbu  sahihi  za kulala wageni  

•  Kushindwa kutoa risiti, hati za madai na kumbukumbu nyinginezo kama sheria inavyotaka  

•   Kumzuia Mkurugenzi au Mwakilishi wa Mkurugenzi katika kufanya kazi

zake zilizowekwa na sheria au Kanuni za Ushuru wa Malazi  

•  Kushindwa kutekeleza Ilani iliyotolewa na Kamishna/mkurugenzi ya kuitwa na kuwasilisha nyaraka zinazohusu nyumba yake ya kulala wageni  

 

•  Kutoa taarifa ya uongo kwenye kumbukumbu yeyote inayotumika kwa ajili ya kudanganya au kushindwa au kukataa kujibu maswali vizuri kwa Afisa

wa Serikali aliyepewa madaraka na sheria hii  

ADHABU

•    Mmiliki atakayetenda mojawapo ya makosa yaliyotajwa hapo juu atalipa faini isiyopungua Tshs. 50,000. kwa Mkrugenzi wa Manispaa na isiyozidi Laki tano (500,000) Mahakamani akipatikana na hatia.  

•  Mmiliki anayekwepa kulipa Ushuru wa Malazi kwa makusudi akikamatwa na kutiwa hatiani atalipa faini isiyozidi shilingi milioni mbili (2,000,000.)  

USIMAMIZI WA BIASHARA NDOGO NDOGO

Uendedhaji wa biashara ndogondogo unasimamiwa na sheria ndogo ya Jiji ya mwaka 1991 (The Dar es Salaam City Town/(Hawking and Street trading) amendment By – law 1999) sheria hii inalenga kuthibiti uharibifu wa Mazingira, kuhatarisha maisha/Afya za wananchi, kuleta sura mbaya ya Mji na uvamizi wa maeneo ya wazi/starehe.

MASHARTI YA KUFANYA BIASHARA

•   Mfanyabiashara awe safi na nadhifu  

      •   Umbo chombo safi cha kufanyia biashara  

      •   Eneo la kufanyia biashara  

•   Kuboresha na kuhifadhi mazingira  

•   Kuwe na eneo la kufanyia biashara linalokubalika kisheria  



MAKOSA

Sheria hii ndogo inamzuia mtu kufanya biashara kwenye maeneo yafuatayo:-

•   Bustani za Jiji /Manispaa  

•  Mbele  za  nyumba  za  Serikali,  Taasisi  za  Fedha,  Ofisi  za  Ubalozi, Mashirika ya Serikali, Kimataifa, Nyumba za Ibada na Taasisi zisizo za Kiserikali (NGOs).  

•   Mashule, Hospitali, Maeneo yaliotengwa kwa kumbukumbu za Kitaifa.  

•   Maeneo yanayozuia mtu kuingia na kutoka kwenye jengo.  

•  Maeneo yenye kumzuia au kuleta usumbufu kwa watembea kwa miguu,na     katika hifadhi ya barabara.

•   Maeneo ya kupumzikia (bus stand) au kuegesha magari.  

•   Kutundika bidhaa kwenye majengo ya watu, Taasisi, Miti, Kuta (Fence)

nguzo za taa, Umeme, vituo vya simu, viti vya kumpumzikia wasafiri.  

•   Kutembeza bidhaa Maofisini.  

ADHABU

Mfanyabiashara atakeyetenda majawapo ya makosa haya akikamatwa atafikishwa  Mahakamani  na  adhabu  yake  ni  faini  au  kifungo  au  vyote  kwa pamoja.

Usajili wa Taxi Cabs chini ya Sheria ndogo ya Jiji (The City of Dar es Salaam

(Registration of Taxi –cabs and Private Hire Vehicles) By-law, 1968

MASHARTI

Mmiliki wowote wa gari ndogo anayetaka kusajili gari lake ni lazima akamilishe masharti yafuatayo:

•   Rangi ya gari iwe nyeupe  

 

•   Iwe imekaguliwa na Polisi wa Usalama barabarani na ripoti ya ukaguzi iwe imekamilika  

 

•   Mmiliki awe amekwisha lipia tozo zote za Mamlaka ya Mapato na kupewa stika  na  leseni  ya  taxi  (sticker  and  Taxi  =-cabs  licence)  kutoka  TRA Pamoja na Bima iliyo hai.

UTARATIBU

Mwombaji anatakiwa kufika na kivuli cha Kadi ya gari na awe ametimiza masharti yaliyotajwa. Atapewa fomu ya maombi ya usajili na atajaza kikamilifu na kuambatanisha:

•   Kivuli cha Kadi ya gari  

 

•   Ripoti ya ukaguzi  

 

•   Stika kutoka Mamlaka ya Mapato  

 

•   Taxi – cab licence kutoka Mamlaka ya Mamlaka ya Mapato  

 

•   Kituo cha kuegesha  

Mmiliki baada ya kukamilisha taratibu atalipa ada ya Tshs. 61,000.00 kwa

mchanganuo ufuatao:

•
Ada ya Maegesho
-Tshs. 36,000.00  
•
Ada ya Usajili
 - Tshs. 20,000.00
•
Ada ya Kituo
 - Tshs. 5,000.00

JUMLA
- Tshs. 61,000.00

Baada ya malipo anapata Hati ya Usajili na namba ya ubavuni.

MAKOSA

•   Kufanya biashara ya taxi-cabs bila ya kusajili  

•   Kuegesha Taxi – cab kwenye Kituo ambacho hakijaainishwa  

•   Kutokuwa na ripoti ya ukaguzi ya Polisi wa Usalama barabarani  

•   Kutokuwa na Leseni ya Taxi-cab 

•   Kutokuwa na Stika  

ADHABU

Anayefanya kosa lolote atakamatwa na Mamlaka inayohusika na kufilishwa kwa kosa hilo.

12


Matangazo

  • TANGAZO LA MRADI WA TACTIC HALMASHAURI YA MJI BARIADI March 09, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI February 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA KAZI YA UDEREVA DARAJA LA II ULIOFANYIKA TAREHE 28/02/2023 February 28, 2023
  • JINSI YA KUBADILISHA TAHUSUSI (COMBINATION) KIDATO CHA TANO June 13, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • ONGEZENI KASI KWENYE KUONYESHA MIRADI ILIYOFANYIKA

    February 07, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA RASIMU YA BAJETI YA MATENGENEZO YA BARABARA NA MADARAJA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 TSHS 2,060,610,000.00

    February 07, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA RASIMU YA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI 2025/2026 BILIONI 29,235,121,948.00

    February 07, 2025
  • ONGEZENI UMAKINI NA MIKAKATI KWENYE UKUSANYAJI WA MAPATO

    February 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Ziara ya Mhe Rais Mjini Bariadi
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Union Day
  • BARIADITC

Tovuti Mashuhuri

  • Watumishi Portal
  • OR-Tamisemi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Along Bariadi-Lamadi Road

    Anuani ya Posta: P. O. Box 526, Bariadi

    Simu ya Mezani: +255 (28) 2700554

    Simu: ******

    Barua Pepe: info@bariaditc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.